Monday 23 February 2015

ANGALIA KILICHOTOKEA LEO NJE YA BUNGE LA UKRAINE WAZICHAPA NJE NJE







Ona kilichotokea katika Nje ya bunge la UKRAINE ,,, je ni demokrasia imezidi au haipo kabisa


JESHI LA POLISI LPATA WASIWASI JUU YA VIKUNDI VYA USALAMA VYAMA VYA SIASA


 

 

  kikundi cha usalama cha CHADEMA



JESHI la Polisi nchini limetangaza kuanza uchunguzi dhidi ya vikundi vyote vya ulinzi na usalama vinavyoanzishwa na vyama vya siasa nchini.
Pamoja na hili limesema kuwa litachunguza kwa kina mafunzo yanayotolewa na vyama hivyo kama yanahusiana na shughuli za kijeshi au laa.
Hatua hiyo ya Jeshi la Polisi imekuja siku moja baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuzindua kikundi cha Ulinzi na Usalama (Red Brigade) katika mikoa ya Kanda za Nyanda za Juu Kusini.
Akizungumza na mwandishai  wa  habari  jijini Dar es Salaam jana, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Ernest Mangu alisema kuwa, sheria za nchi zimeweka wazi namna ya kuwapo kwa vikundi vya ulinzi na usalama na si kila mtu anaweza kuanzisha kikundi chake.
Alisema licha ya baadhi ya vikundi kutambulika lakini vingi hufanya kazi kwa utaratibu na kwa mujibu wa sheria za nchi.
IGP Mangu alisema hatua ya kila chama kuanzisha kikundi chake inaweza kusababisha vurugu hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Alisema kutokana na hali hiyo ni lazima Jeshi la Polisi liwe makini wakati wote kwa kuhakikisha wanafuatilia mwenendo vya vikundi hivyo na madhumuni ya kuanzishwa kwake.
“Tutachunguza vikundi hivyo ili tuweze kubaini mafunzo wanayopewa kama yanafanana na mafunzo ya vikosi vya ulinzi na usalama vinavyofanya kazi kwa mujibu wa sheria za nchi. Katiba ya nchi inavitambua vikosi vya ulinzi na usalama ambavyo vinafanya kazi kwa mujibu wa sheria.
“Kuanzishwa kwa vikundi vidogodogo ndani ya vyama vya siasa ambavyo vinafanya kazi ya ulinzi na usalama vinaweza kuhatarisha amani ya nchi, lazima tuchunguze ili tuweze kubaini mafunzo wanayopewa kama yanafanana na vikosi vya ulinzi na usalama au la, hapo tutajua ukweli zaidi,”alisema IGP Mangu.
Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi alisema katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu wa rais, wabunge na madiwani jeshi la polisi limejipanga kudhibiti vitendo vyote vya uvunjifu wa amani ambavyo vinaweza kuhatarisha hali ya usalama wa nchi na watu wake.
Alisema kutokana na hali hiyo, watahakikisha kuwa vikundi vinavyoanzishwa havifanyi kazi ya ulinzi na usalama kwa sababu siyo jukumu lao.
“Lazima tuwe makini hasa katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu kwa kuhakikisha kuwa vikundi hivi vinavyoanzishwa haviwezi kuhatarisha amani ya nchi,” alisema.
Msajili aonya
Akizungumzia suala hilo, Msajili wa Vyama Vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi alisema kuwa, sheria ya vyama vya siasa hairuhusu kuanzishwa kwa vikundi vya ulinzi na usalama, ila wanasiasa wamekuwa wakitafsiri tofauti.
Alisema kuna mambo mengi yanayofanywa na wanasiasa ambayo wanavunja sheria za nchi, lakini wanashindwa kujirekebisha na kujiona wako sahihi.
Alisema kutokana na hali hiyo, suala hilo ni nyeti sana, hivyo wanatakiwa kuelimishwa kwa kina ili waweze kujua majukumu yao ya chama na shughuli nyingine ambazo haziwahusu.
“Unajua hili suala ni nyeti sana, huwezi kulizungumzia ki uwepesi wepesi, kwa sababu lina upana wake, lakini wanasiasa wanalichukulia kikawaida bila ya kuangalia athari zake baadaye,”alisema Jaji Mutungi.
Aliongeza kuna matatizo mengi ya upotoshaji wa kisheria ndani ya vyama vya siasa, jambo ambalo linaweza kusababisha migongano ya wenyewe kwa wenyewe.
Alisema kutokana na unyeti wa suala hilo hawezi kulizungumzia kwa ufupi kwa sababu kuna masuala ya kisheria ambayo yanapaswa kufafanuliwa kwa kina zaidi ili jamii iweze kutambua ukweli kuhusu suala hilo.
“Lazima ifike kipindi vyama vya siasa vifuate matakwa ya sheria ya nchi kwa sababu ndiyo sheria mama inayoongoza nchi, bila ya kufanya hivyo tutakuwa tunavunja sheria kila siku,”alisema Jaji Mutungi.
Kwa muda mrefu vyama vya siasa hasa vya CCM, Chadema na CUF vimekuwa vitoa mafunzo kwa vijana wake kwa lengo la kuimarisha ulinzi na usalama hasa katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi.
Mbali ya Chadema inayomiliki Red Brigade, CCM inamiliki kikundi cha Green Guard, huku cha CUF ikimiliki kikundi cha Blue Guard.

ANGALIA WANAJESHI WA JKT WALIOKOSA AJIRA WALIVYOENDA KUMJULIA HALI MUHIMBILI BAADA YA KUTEKWA



Mwenyekiti wa JKT, George Mgoba akiwa wodini.
Askari wakiimarisha usalama eneo la 
 Hospitali ya Muhimbili.
Baadhi ya askari wa JKT wakiwasili Muhimbili.
Baadhi ya wanajeshi wa JKT wakiingia hospitalini.
VIJANA mbalimbali ambao walipata mafunzo kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), leo wamekutana katika eneo la Msimbazi Center jijini Dar es Salaam, kisha kuelekea katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kumjulia hali mwenyekiti wao George Mgoba ambaye alitekwa na watu wasiojulikana.
GPL ilifanikiwa kufika eneo la Msimbazi Center walipokusanyika askari hao na baadaye kuelekea Hospitali ya Muhimbili. Hata hivyo, wanahabari walishindwa kuzungumza na mwenyekiti huyo kwa sababu za kiusalama.

VITA VYA URAIS CCM NJE NJE ... VIJANA KWA WAZEE WAPIGANA VIJEMBE









Sadifa Juma Hamisi 

Na Mussa Juma, Mwananchi
Arusha. Wakati joto la urais likizidi kupanda ndani ya CCM kutokana na hofu ya baadhi ya majina mazito ya wagombea wa nafasi hiyo kukatwa kwa mizengwe, vita vya wagombea sasa ni dhahiri baada ya mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM kusema hakuna mtu atakayekatwa bila ya sababu za msingi.
Mjumbe huyo, Sadifa Juma Hamisi, ambaye ni mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), pia alisema umoja huo haujafikia uamuzi wala kumtuma mtu kumdhibiti mwanachama anayetajwa kuwania urais.
Katika siku za karibuni kumekuwapo mjadala mkubwa ndani ya CCM juu ya mtu atakayepitishwa kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho, na ilizidi baada ya Rais Jakaya Kikwete kueleza kuwa mwanachama ambaye atateuliwa na CCM kugombea urais hayumo miongoni mwa waliojitokeza na kuwataka wanachama kuwashawishi watu wenye sifa wajitokeze.
Siku chache baadaye, Dk Raphael Chegeni aliliambia gazeti la Mwananchi kuwa ametumwa na wanachama wa CCM wa mikoa ya Kanda ya Ziwa kwenda kumshawishi Lowassa kujitokeza kuwania urais kuitikia wito wa Rais Kikwete wa kuwataka wanachama kuwashawishi watu wenye sifa kujitokeza.
Hadi sasa, wanachama waliojitokeza kuwania kuteuliwa na CCM kugombea urais ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda, January Makamba (Naibu Waziri wa Sayansi na Teknolojia), Hamisi Kigwangala, na Lazaro Nyalandu ambaye ni waziri wa Maliasili na Utalii.
Lakini pia wako wanaotajwa kuwania urais lakini hawajatangaza ambao ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sita, William Ngeleja, Emmanuel Nchimbi, Mwigulu Nchemba, Stephen Wasira, Bernard Membe na Edward Lowassa ambaye ameibua mjadala kati ya kambi yake na zinazompinga.
Mapema wiki iliyopita, katibu wa uhamasishaji na chipukizi wa UVCCM, Paul Makonda alikaririwa akisema kuwa vitendo vyake vya kumshambulia Lowassa vinatokana na kutumwa na umoja huo kumdhibiti, jambo ambalo limezidisha mjadala kuhusu mteule wa chama hicho.
Kutokana na hofu hiyo, viongozi wa UVCCM na CCM mkoani Arusha wametuma ujumbe wa maneno kwa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa za chama hicho wakitaka wanachama wasifanyiwe kile wanachokiita kuchafuana na vitisho vya baadhi ya wagombea kukatwa kimizengwe.
Ujumbe huo ulitumwa juzi na mwenyekiti wa CCM wa mkoa, Onesmo ole Nangole na mwenyekiti wa UVCCM, Robinson Meitinyiku ambao walitaka Sadifa Juma Hamis kueleza msimamo wa mkoa kwa vyombo hivyo viwili vya maamuzi, na mjumbe huyo wa Kamati Kuu ya CCM aliwahakikishia kuwa hakuna mgombea atakayekatwa kwa “sababu za kijinga”.
Akijibu ujumbe wa viongozi hao, Sadifa aliyekuwa jijini hapa kumsimika kamanda wa vijana wa wilaya ya Arumeru, Mathias Manga, aliwaondolea hofu katika hafla hiyo akisema hakuna mgombea wa urais wa CCM ambaye atakatwa bila sababu za msingi, lakini akawataka vijana kusubiri zamu yao hadi 2025.
Kauli ya Sadifa


“Niwaombeni mwenyekiti wa mkoa na mwenyekiti wa UVCCM, msiogope. Hakuna mtu atakayekatwa kijinga ndani ya Kamati Kuu au Halmashauri Kuu. Kikubwa tufuate maadili. Mimi mchapakazi ndiye nitamtetea,” alisema bila kutaja mgombea anayekusudiwa.Alisema ni lazima kiongozi bora awe na mikakati na dira na upeo wa kuwa na mikakati bora ya kutekeleza ahadi zake kwani hatuwezi kuwa na kiongozi ambaye hana dira wala mikakati.
“Tunataka kiongozi mwenye kujiamini, awe ana vision (dira) na mission (mikakati), msikivu... hatuwezi kuchagua rais ambaye hana sifa hizi,” alisema.
Akizungumzia maombi ya Nangole kuhusu tabia ya kuwachafua baadhi ya wagombea na kuwatisha, Sadifa alisema hakuna kiongozi aliyetumwa na CCM na UVCCM kutukana mtu wala kumtisha.
“Mzee wangu, watu wengi wanajua wanamtaka nani, ukiona mtu anapanda kwenye majukwaa anamchafua mwenzake, ujue huyo ana mapungufu ya malezi, hakuna haja ya kumjibu kwani utaonekana na pia wewe una mapungufu,” alisema.
Akionekana kujibu kauli ya Makonda, Sadifa alisema UVCCM haijatuma mtu amtukane mwingine. Alisema akiwa mjumbe wa Kamati Kuu, hawajawahi kumtuma kiongozi yoyote kumtukana mwanachama mwingine wa CCM.
Alipoulizwa kuhusu hofu hiyo, kwa kifupi katibu wa itikadi na uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema: “Mimi siwezi kuwa msemaji wa Umoja wa Vijana, nikisema niwajibu nitakuwa nimepotoka.”
Mapema wiki iliyopita, Makonda alikaririwa akisema kuwa amekuwa akimshambulia Lowassa, ambaye anatajwa kuwania urais kupitia CCM, kwa sababu ametumwa na umoja huo.
Makonda amekuwa akikaririwa mara kwa mara akisema kuwa Lowassa hafai kuwa mteule wa CCM wa kuwania urais na mikanda ya kauli zake imesambaa kwenye mitandao ya kijamii, jambo lililofanya uteuzi wake kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni uhojiwe na watu wengi na hivyo kujikuta akilazimika kusema ametumwa na umoja wake kumdhibiti waziri mkuu huyo wa zamani.
Katika mazungumzo yake juzi, Sadifa hakutaka kutaja jina la mgombea atakayemtetea wala mtu anayemshambulia, badala yake alisema muda ukifika, kila kitu kitajulikana kwa kuwa watu wanamjua mgombea wanayemtaka.
“Mwenyekiti, dawa ya mjinga ni kukaa kimya, watu wanamjua mtu ambaye wanamtaka. Rais Jakaya Kikwete ni mtu ambaye hatabiriki, hana ushemeji... nyie subirini tu wakati ukifika,” alisema.
Vijana na urais
Akizungumzia vijana ambao wanautaka urais, Sadifa aliwataka kusubiri zamu yao hadi 2025 ili wazee waliopo wamalize muda wao.

Alisema utakapofika mwaka 2025 vijana watakuwa katika nafasi nzuri sana ya kushika uongozi na hawatakubali kuona viongozi wazee wakitaka kupewa nafasi.
“Wazee tutawaomba radhi mwaka wenu ni 2015 hadi 25, mkimaliza hapo, miaka yenu imekwisha, msije tena,” alisema.
Kauli ya Nangole
Awali, Nangole, ambaye aliwahi kusema kuwa Lowassa ni kiongozi msikivu na makini na ambaye ni tegemeo la Watanzania katika kuwaunganisha kuwa kitu kimoja, aliomba Kamati Kuu ipelekewe ujumbe kuwa CCM mkoani Arusha hairidhishwi na matendo ya baadhi ya viongozi kuwatukana na kuwatisha wengine.
Nangole alirejea kauli aliyowahi kuitoa kuwa CCM ni ya wanachama wote na ndani yake hakuna sisimizi au tembo wa kumtisha mwingine ili mradi anafuata taratibu za chama hicho.
Alisema imeibuka tabia ya baadhi ya viongozi wa CCM, kuwatisha wengine na kuwatukana kana kwamba wao ndio wana hatimiliki ya CCM.
Naye mwenyekiti wa UVCCM mkoani Arusha, Robinson Meitinyiku alisema kuna kiongozi mmoja ametoa kauli kuwa mgombea mmoja hata kama akisafishwa na madodoki hawezi kuwa msafi.
Badala yake alisema kiongozi aliyetoa maneno hayo ndiye hawezi kusafishika hata kwa gunzi kwani kuna taarifa aliwahi kusaliti na kujiunga na chama kingine.

MAGAZETI YA LEO JUMATATUTU 23/2/2015


 DSC09824



































http://i1.wp.com/millardayo.com/wp-content/uploads/2015/02/DSC09827.jpg


 .



.


 .

 .

 .


 .

 .

 .


 .


 .

 .

.

 .

 .

 .

 ..

 .



 .


 .

 .

 .

 .

.



















Sunday 22 February 2015

CHADEMA YATIKISA SUMBAWANGA


 

Kati ya mitaa 44 ya sumbawanga mjini chadema mpaka sasa imetangazwa ushindi kwenye mitaa 34 huu ulikuwa ni marudio ya uchaguzi... kwa mahesabu zaidi ya mji mdogo huwo wa sumbawanga nawaachia ccm wapige mahesabu.
Kinachoendelea sumbawanga sasa....
Uchaguzi Mitaa 44 Ya Kata 3 Sumbawanga Mjini Leo Tar 22.02 CCM INA MITAA 4 PAMOJA NA 1 WALOWEKA PINGAMIZI, CHADEMA INA MITAA 39...

GABRIEL MWANG'ONDA NA UCHAMBUZI WA KIUCHUMI SEKTA YA MAFUTA TANZANIA

 



In Tanzania edible oil is the second most expensive commodity that we import after refined petroleum products.
Our balance of payments is not in a good shape because of these two products,Leave alone petroleum products which we might,(just incase we find any) do away with.
Sasa kwa hili la palm oil (mawese) sioni ni wapi tunakwama mpaka tunashindwa kujitosheleza. Mawese Ya Kigoma kwa akina Zitto Kabwe na kwetu kule Kyela yakilimwa kwa ustadi na utaalamu tutaondokana na tatizo kubwa la ajira,tutabakiza fedha zetu nchini,ulali wa biashara za nje utaimarika,serikali itapata fedha nyingi tu kwa njia Ya kodi.
Uthibiti uliopo kwenye sekta Ya sukari basi uwepo hata huku,uwezo tunao lakini sera nazo inafaa ziwe na upendeleo kwetu ili tulime kisasa na kuhakikishiwa soko la ndani na nje.
Mahitaji ni MT-350k kwa mwaka hii ni biashara kubwa kabisa nchini na ku export kabisa,sasa tumebaki kuinunua toka mbali sana..hii product inaweza Kabisa ikawa ni chanzo Cha forex-inawezekana timiza wajibu wako.
Ni ndoto kama ningekua Magogoni
GM

Saturday 21 February 2015

STOP ALBINO KILLINGS,,,,CAMPAIGN




There is more to life than uniformity. .. The Preciousness of Albino is in protecting their lives and rising above the Mediocrity that comes with superstition and the Madness it encompasses.
Other albino species are the beauty of nature, Protect Albinos Tz. Let's make noise about it and ‪#‎StopThisMadness‬












 
























































NYINGE NAZARENO NJIA PANDA KUGOMBEA DODOMA MJINI AU KALENGA




 
 
Nazareno Nyinge: Anasema
"Wakati nafanya tathmini ndogo ya kusimama kupigania jimbo la dodoma mjini naangalia kwa jicho la mwewe jimboni kwangu nilikozaliwa KALENGA ambapo fadhila zimetumika kurithisha madaraka pasipo kujali huruma ya wananchi wanaotaka mabadiliko napata shida sana na cjui nisimame wapi kote hali ngumu

1. wanawake wanapata shida mahospitalini

2. miundombinu kwao ni hadithi husikia kwenye taarifa ya habari tena kupitia radio ya m/kiti wa mtaa

3. huduma za jamii nashukuru kwa kuwa mungu aliweka vyanzo vya maji hivyo wanakunywa maji meupe yasiyo salama

4. kufanya mabadiliko wanatishiwa kutatokea vita

5. kofia na khanga imekuwa ndiyo hongo kwao

6. napata uchungu kuona wanafunzi wanakaa chini mpaka miaka zaidi ya 50 baada ya kuwa huru

7.kenya wanafanya jitihada angalau kila mwanafunzi awe na computer yake wakati tanzania tunasema angalau kila mwanafunzi awe na dawati

nathubutu bila kuwa na maslahi yeyote kwamba sintoacha hata chembe ya sekunde ya muda kupotea nitapigana mpaka mabadiliko ya kweli na ukombozi wa kweli unapatikana

vijana tubadilishe fikra zetu kwa kutokujikitaa sana kushabikia vyama tuweke watu wanaoweza kuleta mapinduzi ya kweli

viwanda kurudisha

rasili mali kupewa nafasi kutumika na wananchi tabaka zote kwa usawa

wananchi kujivunia kile kilichochao daima....young generation forever...

President Kagame meets with Federal Foreign Minister of Germany





President Kagame meets with Federal Foreign Minister of Germany,Frank-Walter Steimmeier during his working visit to Rwanda.
For more pictures: https://www.flickr.com/phot…/paulkagame/…/72157650884180726/

UN:WANAOENDESHA UHALIFU SYRIA KUTAJWA,,,, SOMA HAPO CHINI


 Wanaoendesha uhalifu nchini Syria sasa kutajwa na umoja wa mataifa

Wachunguzi wa Umoja wa Mataifa wanapanga kuchapisha majina ya takriban watu 200 wanaotuhumiwa kuendesha uhalifu wa kivita nchini Syria.
Tume huru ya uchunguzi ya umoja wa mataifa inasema kuwa kumekuwa na ongezeko la uhalifu nchini humno.
Majina yanayojumuisha wakuu wa kijeshi , wasimamizi wa magereza na makamanda wa makundi yasiyokuwa ya serikali yaliyo na silaha tayari yamewasilishwa kwa tume ya haki za binadamu ya umoja wa mataifa.
Serikali ya Syria hatahivyo imekataa kutoa ushirikiano kwa tume hiyo.
Umoja wa Mataifa unasema kuwa zaidi ya watu 220,000 wameuawa nchini Syria na mamilioni ya wengine wamehama makwao wakati wa mazozo wa miaka minne .

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametimia miaka 91 leo

 
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametimia miaka 91 leo.
Yeye sasa ni kiongozi mzee kabisa duniani, na amekuwa madarakani kwa miaka 35.
Sherehe ya siku yake ya kuzaliwa itafanywa juma lijalo.
Anatarajiwa kufanya sherehe kubwa katika uwanja wa golf huko Victoria Falls, inakisiwa sherehe yenyewe itagharimu dola milioni moja.
Maelfu ya watu watahudhuria karamu hiyo, ambapo kutachinjwa ndovu, nyati, paa na simba mmoja.
Shirika la habari la taifa linasema wananchi watalipia dhifa hiyo
Zimbabwe ni moja kati ya nchi maskini duniani.

Friday 20 February 2015

KAULI NZITO YA KADA WA CHADEMA JUU YA MAUUWAJI YA ALBINO



Remija Wa Yesu
Nimesikitishwa sana na mauaji ya mtoto Yohana Bahati!! Mauaji ya kinyama kabisa, ninalaani mauaji haya.
Ninachojiuliza kama serikali inatumia pesa nyingi kujenga mahospitali na kuajiri madaktari, na inasema haiamini katika uchawi, sasa hawa waganga wa kienyeji na wachawi wanatoka wapi? Kwanini wanasajiriwa? Kwanini wapo kwa tiba zipi? Mbona haya mahospitali hawajawahi kutoa rufaa wagonjwa waende kutibiwa kwa waganga wa kienyeji?
Utasikia watasema tuwalinde albino, tuwapeleke kwenye mashule fulani, tusiwaache peke yao, kwanini hawa wachawi wasizuiliwe kufanya kazi zao? Watu wajiishie kwa rahaaa.
Ninachoshangaa na kujiuliza zaidi watanzania wote isipokuwa wachache sana: niliwahi kuambiwa, nilipokuwa mdogo Kingunge tu ndio haamini katika dini hizi, ila sijathibitisha mpaka leo, na katika kukua kwangu mpaka leo sijakutana na MTU mpagani, ila wote sisi ni wakristo na waislamu tena waumini wazuri wa kuhudhuria kwenye nyumba za ibada, inakuwaje hawa waganga wapo na wanapata wateja? Ni Mungu yupi tunayemwabudu? Au ndio michanganyo, mungu baali kidogo na Mungu muumba Mbingu na Nchi kidogo.
Ningekuwa rais ningefutulia mbali waganga wote.
RIP Yohana Bahati kilio cha damu yako kitafika Mbinguni!!!!!

Rais Jakaya Kikwete akabidhiwa rungu la Afrika Mashariki,,,,, Jijini Nairobi

 



Marais Wa Afrika Mashariki Kutoka Kushoto Ni Mh.Pierre Ngurunzinza Wa Burundi,Mh.Jakaya Mrisho Kikwete Wa Tanzania, Mh.Uhuru Muigai Kenyatta Wa Kenya, Mh.Yoheri Museven Wa Uganda na Paul Kagame Wa Rwanda Leo Hii Jijini Nairobi

 

 Rais Paul Kagame Na Hasimu Wake Rais Kikwete Na Mwenyeji Wa Rais Uhuru Wa Kenyatta Kabla ya kikao


Rais Wa Kenya Uhuru Muigai Kenyatta Akimkabidhi Rais Wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete Uwenyekiti wa Jumuia ya Afrika mashariki Leo Hii Jijini Nairobi.

 

Mh.Uhuru Kenyatta akimpokea Mh Kikwete Jijini Nairobi

 

 Rais Wa Kenya Uhuru Akimpokea Rais Wa Uganda Mh. Mseven

 

 Baadhi ya Marais Wa Jumuiaya ya Afrika Mashariki Wakiwa pamoja na makamu wa Rais wa Kenya Mh.Ruto Kabla ya Mkutano

 

 Rais Uhuru Na Pierre Ngurunzinza Wakisalimiana

 
 Rais Uhuru Kenyatta Wakisalimiana na Paul Kagame


Picha kwa hisani ya Nombees toka Nairobi

EMOTIONALIINTELIGENCE CAN BE YOUR PROJECT MOST CRITICAL SUCCESS FACTOR

 Emotional Intelligence Can Be Your Project's Most Critical Success Factor
When a high-profile project fails, news articles are quick to publicize what went wrong, but few care to explain why these projects failed. 
Over the past 20 years, organizations such as the Standish Group have catalogued a wealth of information about the causes of project failure as well as identifying success factors. In the last few years, a new success factor has emerged: emotional maturity or or emotional intelligence (EQ). 
According to Daniel Goleman, the author of Emotional Intelligence, emotional intelligence is made up of five key components: self-awareness, self-regulation, motivation, empathy and social skills. 
When EQ components are evident, a project team will act with a high emotional bank account, the buffer or shield that can protect a team and support project success on a high-risk, high-engagement project. An emotional bank account is a Stephen Covey metaphor for the amount of trust perceived in a relationship.
With a well-funded account balance, project team members feel secure in imagining and executing creative paths to success and issues that arise are remedied efficiently and maturely. Research shows that a more cohesive, high-performing team produces better results. 
But an EQ-deficient environment leaves employees feeling overworked, underappreciated and unwilling to help each other. Quite simply, unhappy team members can hinder the success of a project. 
When the emotional bank account is low, problems arise more easily and can cause project failures, potentially even requiring a complete project turnaround. Unhappy and unproductive teams with little change to spare in their emotional piggy banks can feel like their problems are insurmountable and will disengage from the project. 
Here are a few warning signs that your team may be lacking in emotional intelligence: 
Team members constantly blame others for issues.
You hear victim statements (“I can’t because…”).
Team members are arrogant and not open to the opinions of others.
Members of the team become overambitious and overextended, trying to solve problems they cannot or should not.
Your team is consistently unavailable. 
To effectively build a team’s emotional bank account, start by gauging its emotional state. A team with a healthy, robust emotional bank account knows how to have fun, continuously learn and give and receive quality feedback. If your team needs an emotional intelligence boost, consider taking the following actions: 

1. Enable team members.

The most effective way to ensure a healthy team is to empower its members with resources, ensuring that they understand their roles, responsibilities and expectations. Thriving teams let their members play to their strengths, focusing on the tasks they are uniquely qualified for, as this will bring them satisfaction in their everyday work and help the team achieve its overall goals.
Here’s how: Assess the emotional intelligence and health of your team. Check in regularly with team members to ensure that they feel supported. Targeted surveys can help, provided that there is a clear feedback mechanism. Once the results are compiled, share them, along with an action plan to rectify the areas of concern, with the entire team.  

2. Gain leadership support.

Obtaining a buy-in and engagement from the company's leadership is a critical success factor for any type of project. Through their advocacy, leaders can make consistent small deposits to the team bank account. And when issues and risks arise, the leaders' hands-on support can sustain the emotional bank account when it's needed most.
Here’s how: For leaders to fully support the emotional intelligence of the team, they must visibly demonstrate their commitment to the project's success by acting as sounding boards, encouraging creativity and calculated risk taking in the work's execution and garnering overall support from the organization to clear the path to success. 

3. Create transparency and clear communication.

When transparent relationships between team members exist, communication and overall clarity of the engagement are much easier. This should include transparency about upcoming activities and decision making for the group as a whole.
Here’s how: This is where solid project managers are worth their weight in platinum. Set up communication channels to inform team members about their responsibilities for activities or events that are in the project timeline. And team members with a strong, well-communicated and consistent decision-making process can function with less ambiguity and time-wasting, political maneuvering.  
Working on a team with a well-funded emotional bank account is an enviable experience, one that anyone would be eager to replicate. It allows for a high-functioning team that is both effective and happy -- with a built-in buffer that helps mitigate any speed bumps.
While intelligent and competent teams are always in demand, those that carry a solid emotional bank account will be the ones that consistently achieve success.

Uhuru Kenyata na Paul Kagame wapewa hadhi ya uongozi wa kimasai walipozindua mradi wa kufua umeme Olkaria 14MW in Naivasha


















PRESIDENTS Uhuru Kenyatta and PaulKagame installed as Maasai elders.

MAGAZETI YA LEO TANZANIA